Janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 linaweza kurejesha nyuma mafanikio yaliyopatikana katika kutokomeza ugonjwa wa virusi vya Ukimwi, AIDS, yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la afya, WHO na lile la kukabiliana na UKIMWI, UNAIDS.