Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

UN-Habitat

04 SEPTEMBA 2025

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuletea

-Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi duniani UN-HABITAT lataka wakusanyaji na wachakataji wa taka watambuliwe kwani ni uti wa mgongo wa kuhakikisha mazingira safi na salama mijini

-Katibu MKuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameipongeza Papua New Guinea kwa kuwa kisima cha kuvuna hewa ukaa na kuzitaka nchi za G-20 kuwajibika katika kudhibiti mabadiliko ya tabianchi

Sauti
10'42"

04 OKTOBA 2021

Katika Jarida la Habari hii leo  kutoka Umoja wa Mataifa Assumpta Massoi anakuletea

-Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa antonio Guterres akifungua mkutano wa 15 wa kamati ya Umoja wa Mataifa ya maendfeleo na biashara UNCTAD15 mjini Bridgetown Barbados ametoa wito wa kuhakikisha usawa wa biashara, uwekezaji na na kujikwamua vyema na COVID-19

-Ripoti ya kamati huru ya uchunguzi wa haki za binadamu nchini Libya imesema kuna ushahidi kuwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaoweza kuwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu ulitekelewa nchini humo tangu 2016

Sauti
15'10"

12 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo anold Kayanda kutoka Umoja wa Mataifa anakuletea

-Shirika la afya ulimwenguni WHO leo limetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutousahau ugonjwa wa Ebola pamoja na kwamba inakabiliana na virusi vya Corona hivi sasa kwani kufanya hiyo itakuwa kosa la jinai lenye madhara makubwa ya kibinadamu

-Mradi wa UNICEF wa mafunzo kwa waendesha boda boda ni nuru kwa wanawake wajawazito na watoto wagonjwa nchini Uganda

Sauti
11'36"
Maimunah Mohd Sharif, Mkurugenzi Mtendaji wa UN Habitat akizungumza katika ufunguzi wa siku ya kwanza ya Kikao cha 10 cha Jukwaa la kimataifa la miji, mjini Abu Dhabi, UAE, 8 Februari 2020
UN-Habitat/Waseem Ali

Jukwaa la kimataifa la miji linaonekana kutambua ‘maono ya pamoja’ kuhusu miji ya siku za usoni

Kikao cha kumi cha Jukwaa la Kimataifa la miji, WUF10, mkusanyiko mkubwa zaidi wa dunia kuhusu miji ya siku zijazo, umeanza jumamosi hii mjini Abu Dhabi, mji mkuu wa muungano wa nchi za UAE ambako maelfu ya watu wanashiriki katika majadiliano, kupitia mikusanyiko tofautitofauti inayowakilisha vijana, wanawake, jamii za mashinani, serikali za kitaifa na kikanda pamoja biashara.