Katiba ya Umoja wa Mataifa leo imetimiza miaka 75
Katiba ya Umoja wa Mataifa ambayo ilipitishwa na kutiwa Saini 26 Juni 1945 mjini San Francisco nchini Marekani na mataifa 50, leo inasherehekea miaka 75.
Katiba ya Umoja wa Mataifa ambayo ilipitishwa na kutiwa Saini 26 Juni 1945 mjini San Francisco nchini Marekani na mataifa 50, leo inasherehekea miaka 75.
Katika dunia ambayo imeghubikwa na misukosuko na majanga kama virusi vya Corona au COVID-19, mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi , ongezeko la pengo la usawa na watu kutotendewa haki kwa misingi ya rangi , changamoto yetu ya pamoja kama jumuiya ya kimataifa ni kuyakabilia haya amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, nchi waangalizi na wengineo wametuma ujumbe mzito wa kisiasa wiki hii kwa kutangaza kwamba sahihi 170 sasa zimeidhinisha wito wa Umoja wa Mataifa wa kunyamazisha silaha na kusimama Pamoja dhidi ya tishio la kimataifa la janga la virusi vya corona au CIVID-19.
Katiba ya Umoja wa Mataifa ikiwa inaelekea kutimiza miaka 75 juma hili Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterrres amesema changamoto lukuki zinazoikabili dunia hivi sasa zinahitaji mwongozo ili kuzitatua na mwongozo huo ni katikaba ya Umoja wa Mataifa.
Guterres kupitia ujumbe maalum wa maadhimisho ya miaka 75 ya katiba hiyo amesema leo hii dunia inakabiliwa na majanga , na kote duniani watu wanapaza sauti zao dhidi ya ubaguzi wa rangi.
Katika Jarida la Umoja wa Matafa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameiasa dunia kufuata katiba ya Umoja wa Mataifa inayotimiza miaka 75 wiki hii katika kutatua changamoto za dunia ikiwemo janga la COVID-19
-Nchini Tanzania hospitali ya CCBRT ambayo ina asilimia 6 ya wahudumu wake wenye ulemavu imesema inachukua hatua zote kuwalinda dhidi ya COVID-19 na kutaka serikali kuweka miundombinu ya kuwasaidia watu wenye ulemavu wakati wa janga la COVID-19
Katiba ya Umoja wa Mataifa ikiwa inaelekea kutimiza miaka 75 juma hili Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterrres amesema changamoto lukuki zinazoikabili dunia hivi sasa zinahitaji mwongozo ili kuzitatua na mwongozo huo ni katiba ya Umoja wa Mataifa.
Katika kuelekea maiak 75 ya Umoja wa Mataifa itakayoadhimishwa baadaye mwaka huu , Baraza la Usalama la Umoja huo limeahidi dhamira yake ya kudumisha katiba ya Umoja wa Mataifa ambayo ndio nguzi ya kuanzishwa kwa Umoja huo na pia kwa utulivu wa kimataifa kwa msingi wa sheria za kimataifa.