Siku ya Ukoma Duniani inalenga hatua za kukomesha maambukizi ya ugonjwa huo wenye umri wa zaidi ya miaka 4000
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO linasema katika muongo huu linataka kuondoa maambukizi ya asili ya ukoma na kuna mazingira yanayofaa kutokomeza ugonjwa huo; matokeo yanategemea hatua za haraka na jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa wagonjwa ambao bado hawajafikiwa.