Ukatili wa kijinsia dhidi ya wasichana na wanawake DRC umefikia viwango vya kutisha:UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF leo limetoa wito wa kuongezwa kwa msaada muhimu na wa dharura wa uingiliaji kati na ufadhili ili kukabiliana na ongezeko la visa vinavyoripotiwa vya ukatili wa kingono dhidi ya watoto na wanawake katika jimbo la Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.