Sudan: Wanamgambo waasi wa RSF wahusishwa na ukatili wa kupindukia
- Utekaji wa wasichana na wanawake
- Wanawake na wasichana wanafungwa minyororo
- Matukio 50 ya unyanyasaji wa kingono
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO umewasimamisha kazi baadhi ya walinda amani wake kufuatia ripoti za ukiukwaji mkubwa wa maadili ya kazi.
Walaamu wa Umoja wa Mataifa wameelezea kusikitishwa na ripoti za kuenea kwa vitendo vya ubakaji na ukatili wa kingono nchini Sudan unaodaiwa kutekelezwa na wanamgambo waasi wa kikundi cha Rapid Support Forces (RSF).
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita Umoja wa Mataifa umesenma jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa na kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia. Tupate maelezo Zaidi kutoka kwa Flora Nducha
(TAARIFA YA FLORA NDICHA)
Leo jarida la Umoja wa Mataifa linaangazia siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita, Umoja wa Mataifa umesema jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa, kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia.
Utasikia pia kuhusu maonesha ya athari ziletwazo na kauli za chuki ambapo wawakilishi watatu wa taasisi ya Kina mama wa Srebrenica walitembelea maonesho hayo na kuzungumzia maswahibu yaliyowakumba miaka 28 iliyopita na kuacha vidonda katika mioyo yao.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF leo limetoa wito wa kuongezwa kwa msaada muhimu na wa dharura wa uingiliaji kati na ufadhili ili kukabiliana na ongezeko la visa vinavyoripotiwa vya ukatili wa kingono dhidi ya watoto na wanawake katika jimbo la Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.
Mpango wa umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS leo umetoa taarifa ya kila mwaka ya haki za binadamu na ukatili unaoatjiri raia ambayo inaonyesha kuna ongezeko la asilimia 2 la idadi ya raia waliokatiliwa nchini humo mwaka 2022, licha ya kupungua kwa vitendo vya ukatili kwa ujumla kwa asilimia 27 mwaka 2022 ikilinganisha na mwaka 2021.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, jeshi la Afrika Kusini limepeleka timu yake kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO,ili kuchunguza vijinasaba vya watoto na wanawake waliobakwa na walinda amani ili hatimaye kuthibitisha iwapo watuhumiwa ni walinda amani kutoka Afrika Kusini na kisha watoto hao watambue baba zao na pia kupatiwa malezi.
• Matukio 17 ya ubakaji kila siku jimboni Tanganyika, miongoni mwa wanaobakwa ni watoto.
• Vikundi vyenye silaha vinagombea machimbo ya madini
• UNHCR yataka usalama ili manusura wapatiwe huduma za afya
Jaridani Agosti 13, 2021
Katika Jarida la leo Ijumaa tuna habari muhimu kwa siku ikiwemo hali ya kusikitisha ya ongezeko la vitendo vya ukatili wa kingono nchini DRC pia hali tete nchini Afghanistan. Aidha visa vya saratani barani Afrika vimeongezeka.
Mada yetu kwa kina inamwangazia mwandishi wa habari nchini Tanzania aliyezushiwa kufariki kutokana na COVID-19.
Katika neno la wiki ni uchambuzi we methali heri kujikwaa kidole kuliko kujikwaa ulimi.