Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

#Ukatili wa kingono

Naomie Kianga, si jina lake halisi. Ni manusura wa ukatili wa kingono jimboni kivu kaskazini nchini DRC na ni miongoni mwa wanufaika wa mradi wa ushoni unaotekelezwa na WFP
UN News/George Musubao

Asante kwa UN kwa mafunzo ya ushoni sasa tunahudumia familia zetu – Manusura DRC

Umoja Wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) walitufundisha ushoni na walitupatia cherehani ili tuweze kushona nguo tujitegemee na kusaidia familia yetu sisi wanawake wakimbizi wa ndani na pia manusura wa ukatili wa kijinsia katika kambi iliyoko Goma, amesema Naomie Kianga, ambaye jina lake limebadilishwa kwa usalama na heshima yake.

04 JANUARI 2024

Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa, miongoni wa tuliyokuandalia  ni pamoja na mada kwa kina itakayokupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumsikia manusura wa ukatili wa kingono. Lakini kabla ya hiyo utasikia Muhtasari wa Habari na kama ilivyo ada ya kila alhamisi tunajifuza lugha ya kiswahili na leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia methali isemayo “Mla mbegu huvuna vya wenyewe.”

 

Sauti
11'7"

19 JUNI 2023

Leo jarida la Umoja wa Mataifa linaangazia siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita, Umoja wa Mataifa umesema jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa, kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia.

Utasikia pia kuhusu maonesha ya athari ziletwazo na kauli za chuki ambapo wawakilishi watatu wa taasisi ya Kina mama wa Srebrenica walitembelea maonesho hayo na kuzungumzia maswahibu yaliyowakumba miaka 28 iliyopita na kuacha vidonda katika mioyo yao.

Sauti
14'13"