Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ujerumani

MSC/Marc Muelle

Guterres: Tunahitaji utaratibu wa kimataifa ambao unafanya kazi kwa kila mtu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo katika mkutano wa usalama unaofanyika mjini Munich Ujerumani ametoa wito wa kuwepo utaratibu wa kimataifa ambao unafanya kazi kwa kila mtu. 

Asante Evarist Guterres katika hotuba yake amesisitiza wito huo wa amani na utaratibu wa kisasa wa kimataifa akisema utaratibu wa leo wa kimataifa haufanyi kazi kwa kila mtu, "Kwa kweli, ningeenda mbali zaidi na kusema kwamba haufanyi kazi kwa mtu yeyote." 

Sauti
2'40"
Wadau wa lugha ya Kiswahili wakizungumza na Flora Nducha hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York Marekani.
UN News

Lengo letu ni kuhakikisha kila mtu Afrika anakijua na kukizungumza Kiswahili-Wadau

Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yamewadia ni wiki ijayo tarehe 7 ya mwezi Julai ambapo wadau wote wa kiswahili duniani kuanzia kwenye shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, kwenye Mataifa wazungumzaji wa lugha hii adhimu hadi ughaibuni mambo yatakuwa bambam, lakini hapa kwenye makao makuu ya umoja wa Mataifa maandalizi yamefikia wapi? Na nini kitajiri? Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imewaalika wadau wa Kiswahili hapa kwenye makao makuu kufahamu maandalizi yanaendeleaje.

18 FEBRUARI 2022

Katija Jarida la mada kwa kina hii leo kutoka Umoja wa Mataifa KLeah Mushi anakuletea

-Malawi imetangaza kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa wa polio nchini humo na hivyo kuwa ni tangazo la kwanza la uwepo wa ugonjwa huo barani Afrika katika kipindi cha zaidi ya miaka mitano. 

-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linashirikiana na mamlaka nchini Ethiopia na wadau wake kupatia msaada wa dharura kwa maelfu ya wakimbizi kutoka Eritrea ambao walikimbia kambi ya Barahle na viunga vyake huko jimboni Afar baada ya mapigano kuibuka eneo hilo. 

Sauti
10'36"