Wakati mitandao ya uhalifu kote duniani ikijaribu kusaka mbinu za kunufaika na janga la corona au COVID-19, ni muhimu kwa serikali kushirikiana na kufanyakazi pamoja kwa mujibu wa mktaba wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na usafirishaji haramu wa binadamu, usafirishaji wa silaha na uhalifu miongoni mwa nchi , amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.