Baraza la Usalama lajadili Kukabiliana na Ugaidi na Kuzuia Misimamo mikali ya Ghasia
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameliambia Baraza la Usalama kwamba "anatiwa wasiwasi sana na mafanikio ambayo makundi ya kigaidi yanapata katika ukanda wa Sahel (barani Afrika) na kwingineko," akisisitiza kwamba "kama vile ugaidi unavyowatenganisha watu, kukabiliana nao kunaweza kuleta nchi mbalimbali pamoja."