Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ufadhili kwa ajili ya maendeleo

Programu za misaada ya chakula nchini Chad zinakuza kilimo endelevu na inaimarisha kipato na riziki.
WFP/Giulio d'Adamo

Vita dhidi ya COVID-19 na utimizaji wa SDGs ni mitihani inayohitaji fedha:UN

Mkutano wa ngazi ya juu wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo umefanyika leo Alhamisi ukihusisha Umoja wa Mataifa  na maafisa wawakilishi wa serikali mbalimbali, lengo kubwa likiwa ni kuchagiza msaada wa kimataifa wa fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi zinazoendelea ambazo zimedhoofishwa Zaidi na mlipuko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 katika katika hatua zake za utumizaji wa malengo ya maendeleo endelevu , SDGs.

UN News/Grece Kaneiya

Ufadhili kwa ajili ya SDGs unakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo za kisiasa-UNCTAD

Ripoti ya mwaka 2019 kuhusu kuwekeza kwa ajili ya maendeleo endelevu ya kikosi kazi cha mashirika mbali mbali kuhusu uwekezaji kwa ajili ya maendeleo inaonya kwamba kuchangisha fedha zinazohitajika kwa ajili ya kutekeleza ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endelevu inasalia kuwa changamoto.

Licha ya kwamba kuna ishara za mafanikio, lakini uwekezaji ambao ni muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu, SDGs bado hayajafadhiliwa ipasavyo na mifumo ya kimataifa inakabiliwa na wakati mgumu.

Sauti
3'48"
Ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifajijini New York Marekani
UN/Eskinder Debebe

Mikutano 5 ya kuifuatilia wakati wa UNGA74

Ni mwaka mwingine na wakati mwingine na fursa nyingine ambapo macho na masikio ya dunia yanaelekezwa jijini New york kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa , wakati viongozi wa dunia wakiwasili kushiriki kwenye mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA.