FAO yawaleta pamoja wadau kujadili ubora wa udongo kwa mustakabali wa chakula bora
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO linaendesha kongamano la siku nne kwa njia ya mtandao kujadili masuala mbalimbali kuhusu udongo na mchango wake katika kuhakikisha jamii inapata lishe bora kutokana na mazao yalimwayo kwenye udongo.