Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

udongo

26 JULAI 2022

Hii leo jaridani Anold Kayanda anakuletea Habari kwa Ufupi; Mada Kwa Kina na Mashiani:

Katika Mada kwa Kina anasalia makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambako wiki iliyopita Naibu Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa Amina J, Mohammed alizindua maonesho ya “Ulikuwa umevaa nini? Yakionesha nguo ambazo walivalia manusura wa ukatili wa kingono, kwa kuzingatia kuwa jamii humbebesha lawama ya kubakwa yule aliyebakwa badala ya aliyebakwa kwa kisingizio cha mavazi.

Sauti
12'24"
Wanafunzi wakimwagilia mimea maji kwenye shule ya msingi Laos.
© FAO/Manan Vatsyayana

Bioanuwai ya udongo ina umuhimu mkubwa lakini mchango wake haujapewa uzito unaostahili-FAO 

Katika kuelekea siku ya udongo duniani hapo kesho Desemba 5 shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limesema bayonuai ya udongo ina jukumu muhimu la kuchagia katika uzalishaji wa chakula , kuimarisha lishe, kulinda afya ya binadamu, kupunguza uchafuzi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi , lakini mchango wake mara nyingi haupewi uzito unaostahili. 

FAO/Giulio Napolitano

Udongo una umuhimu mkubwa kwa binadamu

Kuelekea siku ya udongo duniani tunaangazia mradi wa Shirika la chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kupitia mradi wa pamoja wa Kigoma (KJP) wa mafunzo kwa wakazi wa Kigoma nchini Tanzania.

Kwa upande wake Elizabeth Mrema Katibu mtendaji wa sekretarieti ya mkataba wa kimataifa kuhusu masuala ya Bayonuai (CBD) anasisitiza umuhimu wa kutunza bayonuai ya udongo.

Sauti
6'16"
FAO/Marco Longari

Tulinde udongo la sivyo tutakosa chakula- FAO

Hii leo ikiwa ni siku ya udongo duniani, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na kilimo duniani, FAO linataka hatua zaidi kuepusha mmomonyoko wa udongo kwa ajili ya mustakabali bora. Assumpta Massoi na ripoti kamili.

(Taarifa ya Assumpta Massoi)

Mkurugenzi wa FAO anayehusika na masuala ya ardhi na kampeni ya siku ya leo, Eduardo Mansur, amesema udongo ambao unahifadhi robo ya bayonuai na kuchangia asilimia 95 ya chakula, hivi sasa unakabiliwa na hatari kubwa.

Sauti
1'18"