Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamesema janga la mlipuko lililotokea Beirut Lebanon Agosti 4 mwaka huu na kusababisha vifo vya watu wengi na kujeruhi wengine kwa maelfu, linahitaji uchunguzi huru na wa haraka ambao utazingatia wajibu wa kimataifa wa haki za binadamu, utakaotanabaisha majukumu ya mlipuko huo na hatimaye kufikia kupata haki na uwajibikaji kwa wahusika.