Mashirika zaidi ya sita ya kimataifa yakiongozwa na Umoja wa Mataifa likiwemo shirika la fedha duniani IMF, Benki ya Dunia na shirika la biashara duniani WTO kwa pamoja wametoa tahadhari katika ripoti yao mpya wakionya kwamba mifumo ya fedha ya kitaifa na kimataifa isipofanyiwa marekebisho na kufufuliwa basi itakuwa ndoto kwa serikali duniani kutimiza ahadi ya masuala muhimu kama kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kutokomeza njaa ifikapo 2030.