29 SEPTEMBA 2023
Hii leo jaridani tunaangazia utupaji wa chakula, na uchaguzi ujao nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Uganda na mashinani nchini DRC, kulikoni?.
Hii leo jaridani tunaangazia utupaji wa chakula, na uchaguzi ujao nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Uganda na mashinani nchini DRC, kulikoni?.
Wakati nchi ya Sudan Kusini ikijiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza kabisa tangu ipate uhuru, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendesha makongamano na vyama vya siasa nchini humo.
Ikiwa imesalia miezi 15 mpaka uchaguzi ufanyike hapo Desemba 2024 UNMISS wanasema lengo la kuandaa makongamano hayo nikujenga utamaduni wa kuwa na mazungumzo thabiti, kutatua changamoto zinazowakabili kuhusu utawala bora na kujenga kuaminiana miongoni mwa wanasiasa na jamii wanazozitumikia.
Wakati nchi ya Sudan Kusini ikijiandaa kushiriki katika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza kabisa tangu ipate uhuru, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendesha makongamano na vyama vya siasa nchini humo.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Sudan Kusini na mradi wa maji nchini Rwanda. Makala tunasalia huko huko Sudan Kusini na Mashinani tunakupeleka nchini Zimbabwe, kulikoni?
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika.
Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO.
Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza wananchi wa kenya kwa kupiga kura kwa amani wakati wa Uchaguzi Mkuu wan chi hiyo uliofanyika hapo jana Agosti 9, 2022
Ucheleweshaji unaoendelea wa mchakato wa uchaguzi nchini Somalia unaendelea kukwamisha maendeleo katika maeneo mengine muhimu na kukwamisha mafanikio ya vipaumbele vya kitaifa zaidi ya uchaguzi.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Amina J. Mohammed, amehitimisha ziara yake ya Afrika Mashariki na pembe ya Afrika kwa kutembelea nchi ya Somalia na kuelezea mshikamano wake na wito kwa wanawake wa Somalia kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu.