Mashirika ya UN yasaidia mamilioni ya waathirika wa kimbunga Goni Ufilipino
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu nchini Ufilipino wanashikamana ili kuzisaidia jamii zilizoathirika vibaya na kimbunga Goni ambacho kimekumba nchi nzima na kuacha uharibifu mkubwa.