Pigeni marufuku uvutaji wa sigara aina zote shuleni ili kuwalinda vijana – WHO
Leo, ili kusaidia kulinda afya ya Watoto, Shirika la Umoja wa Matafa la Afya Ulimwenguni limetoa machapisho mawili mapya, “Uhuru dhidi ya tumbaku na nikotini: mwongozo kwa shule,” na “zana za shule zisizo na nikotini na tumbaku.”
26 SEPTEMBA 2023
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Félix-Antoine Tshisekedi Tshilombo alihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kutangaza kuwa uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika nchini humo mwishoni mwa mwaka huu, utafanyika kama ilivyopangwa. Alisema tayari Tume Huru ya Uchaguzi nchini DRC, CENI [SENI] imeshachapisha majina ya wagombea na michakato mingine inaendelea.
31 JULAI 2023
Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Leah Mushi akimulika masuala ya afya hususan mafanikio ya será za kudhibiti uvutaji sigara na tumbaku; elimu kwa watoto waliokosa fursa huko Kenya; nishati salama nchini Tanzania na ujumbe wa Romeo George mwanaharakati wa SDGs.
Sera ya kuzuia uvutaji sigara hadharini yaleta manufaa kwa umma.
Miaka 15 baada ya Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO kuanzisha sera ya kulinda umma kutoathirika na uvutaji wa sigara unaofanywa na mtu mwingine, zaidi ya watu bilioni 5.6 wamenufaika na sera hiyo ulimwenguni kote, imesema ripoti mpya ya shirika hilo iliyotolewa leo.
Tuzo kwa Sprina mkulima aliyeachana na na kilimo cha tumbaku na kugeukia maharage
31 MEI 2023
Hii leo katika jarida Anold Kayanda anamulika kwa kiasi kikubwa siku ya kutokomeza matumizi ya tumbaku duniani halikadhalika hatua ya kupunguza mgao wa chakula kwa wakimbizi walioko nchini Tanzania.
Kilimo cha maharage chamwondoa Sprina kwenye ‘utumwa’ wa tumbaku
Wahenga walinena mcheza kwao hutunzwa na ndivyo ilivyo hii leo kwa Sprina Robi Chacha, mkulima huyu nchini Kenya ambaye suluba na madhara ya kilimo cha tumbaku alichojifunza na kukitekeleza tangu akiwa mdogo, vilisababisha aachane na kilimo hicho na kujikita na kilimo cha maharage yenye madini ya chuma.
26 MEI 2023
Jaridani hii leo tunaangazia ripoti kuhusu matumizi ya tumbaku na wakimbizi wa Sudan. Makala tunaangazia mauaji ya kimbari nchini Rwanda na mashinani tutakupeleka nchini Chad, kulikoni?
FAO yawasaidia wakulima wa tumbaku Kenya, kuhamia katika mazao mbadala
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeimarisha afya ya wakulima wa kaunti ya Migori. Hii ni baada ya kuzindua machi Mwaka huu mradi wa kilimo mbadala unaolenga kusitisha kile cha tumbaku. Kwa ushirikiano wa WHO na WFP, FAO inajivunia mafanikio kwani afya za wakulima wa Migori zimeimarika baada ya kuacha kilimo cha tumbaku na kukiongeza kipato chao.