Chuja:

Tsunami

Mlipuko wa volkano na Tsunami ya Tonga umeweka wazi mazingira hatarishi ya visiwa vidogo na Mataifa yanayoendelea (SIDS).
© Konionia Mafileo

UNICEF na serikali ya Japan kuwanusuru walioathirika na Tsunami na volcano Tonga 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na serikali ya Japani wametangaza ushirikiano mpya wa kuchangia dola milioni 1.25 kuisaidia serikali ya Ufalme wa Tonga kuhakikisha kuwa takriban watu 19,250 wakiwemo watoto 10,000 walioathiriwa na mlipuko wa volcano na tsunami hivi karibuni wanapata maji safi ya kutosha ya kunywa, mazingira safi , pamoja na afya njema. 

05 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu Tsunami, na kama ilivyo ada leo ni mada kwa kina ambapo tunaangazia vijana na mchango wao katika mabadiliko ya tabianchi wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa COP26 ukiendelea huko Glasgow Scotland. 

Flora Nducha amezungumza na mmoja wa vijana wanaharakati wa mazingira kutoka nchini Kenya na mshindi wa tuzo ya shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP ya champion of the Earth 2020 kutokana na kampuni yake ya Change Makers kubadili taka za platiki kuwa tofali.

Sauti
13'7"