Tetemeko la ardhi Afghanistan limewaacha wanawake na wasichana katika janga la muda mrefu: UN Women.
Wanawake na wasichana ambao bado wanateseka kufuatia tetemeko kubwa la ardhi hivi karibuni nchini Afghanistan wanakabiliwa na mateso makubwa zaidi wanapojaribu kujenga upya maisha yao bila msaada wa kutosha kutoka kwa jamii ya kimataifa, amesema Susan Ferguson, Mwakilishi Maalum wa shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake nchini Afghanistan, UN Women, akizungumza na waandishi wa habari hii leo huko Geneva Uswisi.