Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

tetemeko la ardhi

Mama akiwa amembeba mtoto wake katika kijiji cha Ahmad Abad huko Herat, magharibi mwa Afghanistan, ambacho sehemu kubwa iliharibiwa na tetemeko la ardhi.
© UNICEF/Osman Khayyam

Tetemeko la ardhi Afghanistan limewaacha wanawake na wasichana katika janga la muda mrefu: UN Women.

Wanawake na wasichana ambao bado wanateseka kufuatia tetemeko kubwa la ardhi hivi karibuni nchini Afghanistan wanakabiliwa na mateso makubwa zaidi wanapojaribu kujenga upya maisha yao bila msaada wa kutosha kutoka kwa jamii ya kimataifa, amesema Susan Ferguson, Mwakilishi Maalum wa shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake nchini Afghanistan, UN Women, akizungumza na waandishi wa habari hii leo huko Geneva Uswisi.

08 APRILI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika shughuli za shirika lisilo la kiserikali la KINNAPA Development Programme la huko nchini Tanzania katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu likijikita zaidi katika usawa wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani:

Sauti
11'50"
Mvulana akiwa ameshikilia vifaa vya kujisafi vilivyotolewa na UNICEF.
© UNICEF/Nyan Zay Hte

UN yaendelea kutoa msaada kwa watu wa Myanmar

Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wa misaada ya kibinadamu leo wamesema wanaendelea kuwasaidia watu wa Myanmar na mahitaji ya msingi baada ya tetemeko kubwa la ardhi la Ijuma iliyopita ambapo idadi ya waliopoteza maisha sasa ni zaidi ya 2,800, maelfu wamejerihiwa na mamia bado hawajulikani wako.

Msaada wa dharura wa chakula wa WFP wawafikia manusura wa tetemeko la ardhi huko Pyinmana, Myanmar.
© WFP/Diego Fernandez

UN yaongeza msaada wakati operesheni za uokozi zikiendelea Myanmar kufuatia tetemeko la ardhi

Baada ya tetemeko kubwa la ardhi  la ukubwa wa 7.7 katika kipimo cha Richa kuitikisa Myanmar mwishoni mwa wiki, operesheni za uokoaji zinaendelea huku waokoaji wakiharakisha kuwaokoa wale waliokwama chini ya vifusi vya majengo yaliyoanguka wakati mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yakiongeza msaada unaohitajika haraka.