Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema anaumia na kupata uchungu mkubwa moyoni kufuatia hali ya machafuko inayoendelea Ethiopia nchi anakotoka ,na amertoa wito kwa pande zote katika mzozo kufanya kila liwezikanalo kwa ajili ya kurejesha amani na kuhakikisha ulinzi wa raia na pia kutoa fursa za huduma za afya na misaada ya kibinadamu kwa wale wanao ihitaji.