TANZBATT9

TANZBATT9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania walenga kuhamasisha amani DRC kupitia Kiswahili 

Kikundi cha tisa cha walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-9, kinachohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimeanza kusambaza daftari na vifaa vingine vya shule kwa watoto katika maeneo ya Mavivi huko BENI mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa lengo la kuwahimiza wanafunzi hao kuzungumza lugha ya Kiswahili ili wakimaliza shule waweze kuwasiliana na mataifa mengine.

Sauti
4'27"
© MONUSCO

Mkutano wafanyika kati ya walinda amani na viongozi wa jamii katika harakati za kuimarisha usalama

Kuelekea siku ya kimataifa ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa na katika kuendeleza jukumu la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  vikosi vya ulinzi wa amani kutoka Tanzania yaani TANZBATT 9 na kikosi cha utayari TANZANIA QRF2 vimefanya kikao cha Urafiki baina yao na uongozi wa raia wa nchi hiyo katika maeneo ya uwajibikaji wa vikosi hivyo.

Sauti
3'17"

17 MACHI 2022

Miongoni mwa yaliyomo leo katika jarida letu la Habari linaloletwa kwako na Leah Mushi

- Mswada mpya unaopendekewa Uingereza kuhusu uhamiaji hauna tija kwa wakimbizi, waomba hifadhi na wahamiaji yaonya ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa na kutoa raia kwa serikali ya nchi hiyo kuufikiria upya

-Huko Gambia mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa la ufadhili kwa kilimo IFAD waleta nuru kwa wakulima wa mpunga ambao pia wanafanya biashara

Sauti
13'49"