Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

TANZBATT 9

Credit: TANZBATT9/ Denisia Lihaya

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania huko DRC wakabidhiana lindo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC walinda amani kutoka Tanzania kikosi cha 9 wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wanaendelea kushika doria na kulinda raia katika jimbo la Kivu Kaskazini ambapo wiki hii kikosi cha 9, TANZBATT 9 kimemaliza muda wake na kukabidhi majukumu kwa kikosi cha 10, TANZBATT 10. Je nini kimejiri katika makabidhiano hayo ? Kapteni Denisia Lihaya, Afisa habari wa TANZBATT 9 kabla ya kurejea nyumbani ametuandalia ripoti  hii ya makabidhiano. 

Sauti
4'9"

10 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia taarif aya UNICEF kuhusu kipindupindu, na ziara ya Baraza la Usalama DR Congo. Makala tutasalia huko huko DR Congo kushuhudia maadhimisho wa makabidhiano kati ya TANZBATT 9 na TANZBATT 10, na mashinani tukuletea ujumbe kutoka CSW67.

Sauti
12'11"
TANZBATT 9

TANZBATT 9 wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, Kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 katika doria ya barabara ya Mbau-Kamango
TANZBATT 9

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. 

Sauti
1'45"

16 JANUARI 2023

Ni Jumatatu tarehe 16 ya mwezi Januari mwaka 2023 na jaridani tunakuletea habari za machungu kutoka DRC pamoja na za kazi ya walinda amani nchini humo. Makala tunakuletea simulizi ya mkimbizi kuhusu safari kutoka Venezuela hadi Chile, na mashinani tunakwenda nchini Somalia, kulikoni?

Sauti
11'
TANZBATT 9 / Private Sosper Msafiri

TANZBATT 9 nchini DRC wahitimisha kampeni ya Amani na Afya kwa kukabidhi jengo

Kikosi cha 9 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupitia Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo - MONUSCO wamehitimisha kampeni yao ya Afya na Amani iliyoanza tarehe 3 mwezi huu wa January ambapo  wamekabidhi jengo kwa ajili ya mahali pa wagonjwa na wahudumu wa afya kula chakula katika Kituo cha Afya cha Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
3'55"
Walinda amani kutoka Tanzania waanzisha kampeni ya "Afya na Amani" nchini CRC
Picha: MONUSCO

Baada ya Mavivi, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Sauti
2'13"
Picha: MONUSCO

TANZBATT 9 waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC

Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
5'37"
Walinda amani wa UN kutoka Tanzania waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC
Picha: MONUSCO

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC

Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
5'37"
TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo

Kutanguliza majadiliano katika kutatua matatizo ya ukosefu wa amani utarejesha amani DRC: Meja Jenerali Simuli

Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli ambaye ni Mkuu wa Utumishi katika Jeshi la Tanzania ametoa wito kwa Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kutanguliza majadiliano katika kutatua matatizo yao ya ukosefu wa amani. 

Meja Jenerali Simuli ametoa wito huo alipoongoza ujumbe wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika ziara yao nchini DRC ili kujionea shughuli za mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO ambamo kwa nyakati tofauti, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wamekuwa wakihudumu katika vikosi mbalimbali kikikwemo cha kujibu mashambulizi, FIB. 

Audio Duration
1'46"