Walinda amani wa UN kutoka Tanzania huko DRC wakabidhiana lindo
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC walinda amani kutoka Tanzania kikosi cha 9 wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wanaendelea kushika doria na kulinda raia katika jimbo la Kivu Kaskazini ambapo wiki hii kikosi cha 9, TANZBATT 9 kimemaliza muda wake na kukabidhi majukumu kwa kikosi cha 10, TANZBATT 10. Je nini kimejiri katika makabidhiano hayo ? Kapteni Denisia Lihaya, Afisa habari wa TANZBATT 9 kabla ya kurejea nyumbani ametuandalia ripoti hii ya makabidhiano.