Skip to main content

Chuja:

TANZBATT-8

17 MACHI 2022

Miongoni mwa yaliyomo leo katika jarida letu la Habari linaloletwa kwako na Leah Mushi

- Mswada mpya unaopendekewa Uingereza kuhusu uhamiaji hauna tija kwa wakimbizi, waomba hifadhi na wahamiaji yaonya ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa na kutoa raia kwa serikali ya nchi hiyo kuufikiria upya

-Huko Gambia mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa la ufadhili kwa kilimo IFAD waleta nuru kwa wakulima wa mpunga ambao pia wanafanya biashara

Sauti
13'49"

28 MEI 2021

Katika Jarida la mada kwa kina hii leo Leah Mushi anakuletea
-Leo ni siku ya kimataifa ya hedhi salama ujumbe ukiwa Hatua na Uwekezaji katika Hedhi salama, wakati huu ambapo suala la hedhi linachukuliwa na jamii kuwa ni ugonjwa au mkosi na hivyo kuwakosesha watoto wa kike haki ya kupata huduma ya kujisafi wakati wa mzunguko wa hedhi kila mwezi.

Sauti
12'21"
Mwanamke akiwa amebeba mwanaye mgongoni akielekea nyumbani katika jimbo la Kivu Kaskazini DRC. Hali ya usalama jimboni humo bado ni tete, huku raia wakilipa gharama kubwa ya machafuko yanayofanywa na makundi yenye silaha (Kutoka maktaba)
OCHA/Ivo Brandau

Juhudi za UN kurejesha amani zapongezwa DRC

Shughuli za ulinzi wa amani zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO na jeshi la serikali ya DRC, zimepongezwa na viongozi wa dini pamoja na wananchi wa mji wa Mutwanga ulioko katika eneo la Rwenzori jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
2'35"
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

TANZBATT_7 yatamatisha jukumu lao DRC, TANZBATT_8 yapokea kijiti

Kikosi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT_7 kwenye kikosi maalum cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimetamatisha jukumu lake rasmi na kukabidhi bendera kwa kikosi cha 8 au TANZBATT_8. Shuhuda wetu kutoka Beni, jimboni Kivu Kaskazini ni Luteni Issa Mwakalambo, afisa habari wa TANZBATT_7. 

Sauti
3'19"

16 Februari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha aanza na ombi la dola milioni 222 kwa ajili ya wakimbizi wa Burundi waliosaka hifadhi nchi jirani za Tanzania, DRC na Rwanda. Kisha ni Burkina Faso ambako huko afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa amefika na kujionea hali halisi ya madhila yanayokumba wakimbizi wa ndani waliofurushwa majimbo ya Kusini Magharibi na Kaskazini Magharibi kutokana na ghasia.

Sauti
13'12"