Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

TANZBAT8

Luteni Kanali Barakaeli Mley (kulia) akipokea bendera ya Tanzania kutoka kwa Luteni Kanali Fortunatus Nassoro wakati TANZBATT 8 ikikabidhi majukumu ya ulinzi wa amani nchini DRC kwa TANZBATT 9. (Machi 8, 2022)
Kapteni Denisia Lihaya/TANZBATT 9

Tunaondoka DRC tukiwaachia usalama katika maeneo ambayo yalikuwa hayapitiki - TANZBATT 8

Kikosi cha 8 cha wanajeshi kutoka Tanzania, TANZBATT 8 ambacho kimekamilisha muda wake wa kuhudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, MONUSCO,  kimesema kinajivunia kuondoka nchini humo kikiwa kimesaidia kuleta amani katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo ya barani Afrika ambayo imegubikwa na mizozo kwa muda mrefu.

Gwaride la walinda amani wa Tanzania nchini DRC kabla ya kutunukiwa  nishani za Umoja wa Mataifa
Kapteni Tumaini Bigambo

Walinda amani wa Tanzania nchini DRC watunukiwa nishani za Umoja wa Mataifa

Walinda amani kutoka Tanzania, Kikosi cha 8 cha kujibu mashambulizi kinachohudumu katika ulinzi wa amani chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, FIB MONUSCO wametunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa katika sherehe zilizopambwa kwa gwaride maalum lililoandaliwa na kikosi hicho. Afisa habari wa TANZBATT8, Kapteni Tumaini Bigambo alikuwepo katika hafla hiyo ana ametuandalia ripoti ifuatayo.

Sauti
2'36"

06 OKTOBA 2021

Leo katika Jarida la Umoja wa Mataifa Assumpta Massoi anakuletea

-Janga la utapiamlo limefurutu ada nchini Afghanistan , huku mabadiliko ya tabianchi na vita vinadhidisha madhila kwa watoto na familia zao yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa la UNICEF na WFP

-Mradi wa uvuvi wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO ujulikanao FISH4ACP baada ya kushamiri Kigoma Tanzania sasa umehamia mkoani Katavi kuwaletea nuru wavuvi

Sauti
14'24"