Maelfu ya watu hupoteza maisha kila mwaka kutokana na kutopata tahadhari ya mapema ya majanga yatokanayo na hali ya hewa kama vimbunga, mafuriko, na hata matetemeko ya ardhi. Ili kuokoa maisha shirika la Umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO sasa linachukua hatua likishirikiana na nchi mbalimbali kuhakikisha tahadhari inachukuliwa mapema.