Skip to main content

Chuja:

Takwimu

Uzalishaji wa mtama katika Bonde la Sourou nchini Burkina Faso unaboreshwa na umwagiliaji wa maji.
© FAO/Jeanette Van Acker

FAO yataka nchi kuwa na takwimu za masuala ya kilimo na chakula

Ulimwengu ukiwa katika nusu ya utekelezaji wa Ajenda ya mwaka 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema mafanikio mengi yaliyofikiwa yanayohusiana na chakula na kilimo yamedumaa au yamebadilika, na hivyo kuongeza changamoto katika kutokomeza umaskini na njaa, kuboresha afya na lishe, na kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

© UNICEF Moldova

Rais wa Tanzania atoa takwimu za wagonjwa wa COVID-19

Wakati shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika likionya kuwepo kwa wimbi la tatu la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 barani Afrika, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema sasa taifa hilo lina wagonjwa zaidi ya 100 na tayari taratiu zinafanyika ili kuingia chanjo ya COVID-19.
Rais Samia amesema hayo Jumatatu juni 28 2021 wakati akijibu swali wakati wa mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es salaam.

Sauti
2'16"
UN News

Guterres: Takwimu ni muhimu katika kukabiliana na changamoto za sasa duniani

Katika kuadhimisha siku ya takwimu duniani leo tarehe 20 mwezi Oktoba,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema takwimu ni muhimu sana katika kuunda sera kwa kuzingatia ushahidi sahihi na kwamba

“Takwimu zinazokwenda na wakati, za kutegemewa na za kuaminika, zinatusaidia kuelewa mabadiliko ya dunia tunayoishi na kuchagiza mabadiliko yanayohitajika ili kuhakikisha hatumwachi yeyote nyuma.” 

Sauti
1'2"