FAO yataka nchi kuwa na takwimu za masuala ya kilimo na chakula
Ulimwengu ukiwa katika nusu ya utekelezaji wa Ajenda ya mwaka 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema mafanikio mengi yaliyofikiwa yanayohusiana na chakula na kilimo yamedumaa au yamebadilika, na hivyo kuongeza changamoto katika kutokomeza umaskini na njaa, kuboresha afya na lishe, na kupambana na mabadiliko ya tabianchi.