Kwa mara ya kwanza IOM yatoa takwimu za waathirika na wahalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu
Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiani IOM leo kwa mara ya kwanza limetoa takwimu zinazopatikana hadharani zikiunganisha maelezo mafupi ya waathirika na wahalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu huku zikihifadhi wasifu na faragha ya manusurika.