Shirika la Chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limezindua mradi mpya wa dola milioni 7.1 unaosaidiwa na mfuko wa mazingira duniani, (GEF) kuwezesha upatikanaji wa takwimu kuhusu misitu, zilizo za uwazi na haswa zinazosaidia nchi zinazoendelea kutekeleza makubaliano ya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi.