Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

tabianchi

Wajumbe wawasili katika mkutano wa COP28 kuhusu hatua za hali ya hewa.
© UNFCCC/Kiara Worth

HABARI KWA UFUPI

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 umefungua pazia rasmi mjini Dubai katika Falme za nchi za Kiarabu kwa kuwaleta Pamoja wajumbe zaidi ya 60,000 kuangalia jinsi ya kuongeza hatua, fursa ya nyenzo za kujenga mnepo ikiwemo makubaliano ya kuanzishwa mfuko wa hasara na uharibifu ambayo yamepitishwa kwenye mkutano huo na pia kutumia ubunifu kudhibiti janga hilo.

Watoto wakisimama kwenye maji ya mafuriko katika Jimbo la Borno, Nigeria.
© UNICEF/Vlad Sokhin

Nigeria: Maadhimisho ya Siku ya Watoto Duniani  yaangazia athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watoto

Ikiwa leo ni siku ya mtoto duniani, nchini Nigeria wametumia siku hii kutathmini athari wanazozipata watoto kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Katika taifa hilo lililopo Afrika Magharibi lenye jumla ya watu milioni 233 watoto wanachukua asilimia 51 ya taifa hilo ndio maana mashirika ya Umoja wa Mataifa , serikali na wadau wengine wakaona haja ya kutumia siku hii kuzungumza namna bora ya kuwasaidia. 

Unsplash/Andreas Chu

Mataifa lazima yaende mbali zaidi kuliko ahadi za sasa kutokomeza uzalishaji wa Hewa Chafuzi - UNEP

Wakati joto la ulimwengu na uzalishaji wa hewa chafuzi vikivunja rekodi katika mwaka huu wa 2023, Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) ya Pengo la Uzalishaji hewa chafuzi iliyotolewa leo Novemba 20 mjini Nairobi Kenya imeeleza kwamba imegundua kuwa ahadi za sasa chini ya Mkataba wa Paris zinaweka ulimwengu kwenye mstari wa ongezeko la joto la nyuzi joto 2.5 hadi 2.9 za Selsiasi zaidi ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda katika karne hii. 

Sauti
2'12"
Msichana mdogo nchini Zimbabwe anakunywa maji safi na salama kutoka kwenye kisima kilichorekebishwa kwa msaada wa Umoja wa Mataifa.
© UNICEF/Karin Schermbrucker

Ripoti: Mtoto 1 kati ya 3 anakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji - UNICEF

Mtoto mmoja kati ya Watoto watatu au sawa na watoto milioni 739 duniani kote - tayari wanaishi katika maeneo yaliyo na uhaba mkubwa au wa juu sana wa maji, na mabadiliko ya tabianchi yanatishia kufanya hali hii kuwa mbaya zaidi, imebainisha ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu kwa saa za New York, Marekani.

Sauti
1'49"