Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Taarifa za dharura

UN Photo/Rick Bajornas)

Watu 17 wauawa katika ghasia huko DRC

Huko Kinshasa, mji mkuu wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, kumetokea mapigano kati ya waandamanaji na vikosi vya usalama ambapo watu 17 wamefariki dunia, miongoni mwao raia 14 na polisi watatu.

Vyombo vya habari vinaripoti kuwa mapigano hayo yametokea majira ya leo asubuhi kabla ya maandamano ya kutaka Rais Joseph Kabila ajiuzulu, maandamano ambayo yalifutwa na serikali.

Kufuatia ripoti hizo za vifo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea wasiwasi wake juu ya ghasia hizo Kinshasa na kwenye maeneo mengine ya DR Congo akilaani ghasia zilizotokea.

Huduma za amani na kiutu za UM katika Kenya

Ripoti za UM wiki hii zimethibitisha ya kuwa hali ya usalama Kenya, inaendelea kuwa tulivu, kufuatia wiki kadha za machafuko na vurugu liliofumka katika sehemu mbalimbali za nchi baada ya siotafahamu kuzuka juu ya matokeo ya uchaguzi uliofanyika Disemba mwaka jana.