Watu 17 wauawa katika ghasia huko DRC
Huko Kinshasa, mji mkuu wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, kumetokea mapigano kati ya waandamanaji na vikosi vya usalama ambapo watu 17 wamefariki dunia, miongoni mwao raia 14 na polisi watatu.
Vyombo vya habari vinaripoti kuwa mapigano hayo yametokea majira ya leo asubuhi kabla ya maandamano ya kutaka Rais Joseph Kabila ajiuzulu, maandamano ambayo yalifutwa na serikali.
Kufuatia ripoti hizo za vifo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea wasiwasi wake juu ya ghasia hizo Kinshasa na kwenye maeneo mengine ya DR Congo akilaani ghasia zilizotokea.
Viongozi wa kimataifa wanaohudhuria COP15 wamo mbioni kuharakisha mapatano kabla ya mwisho wa wiki
Viongozi wa kimataifa, wamo mbioni, wakijaribu kukamilisha mazungumzo ya kuleta itifaki mpya, Ijumaa ijayo, itakayoyasaidia Mataifa Wanachama kudhibiti kihakika, madhara yanayochochewa na hali ya hewa ya kigeugeu.
Huduma za amani na kiutu za UM katika Kenya
Ripoti za UM wiki hii zimethibitisha ya kuwa hali ya usalama Kenya, inaendelea kuwa tulivu, kufuatia wiki kadha za machafuko na vurugu liliofumka katika sehemu mbalimbali za nchi baada ya siotafahamu kuzuka juu ya matokeo ya uchaguzi uliofanyika Disemba mwaka jana.
Mchango wa UM kuhudumia amani na misaada ya kiutu Kenya
Timu ya Mashirika Wakazi ya UM katika Kenya imeripoti hali, kwa ujumla, nchini, sasa hivi, inaendelea kuwa shwari na tulivu, isipokuwa katika miji ya Eldoret na Kericho ambako hali huko tumearifiwa bado ni ya kigeugeu na inatia wasiwasi.~
Pagination
- 1
- 2