Wazee wachoshwa na umwagaji damu DRC na Sudan wataka hatua za haraka kukomesha vita
Viongozi wa dunia wamesisitizwa kuwalinda raia na kutanguliza haki za binadamu mbele wakati migogoro ikizidi kuongezeka duniani.
Viongozi wa dunia wamesisitizwa kuwalinda raia na kutanguliza haki za binadamu mbele wakati migogoro ikizidi kuongezeka duniani.
Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, ametangaza tahadhari kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kibinadamu Darfur Kaskazini, baada ya kutembelea Tawila na Korma ambako maelfu ya familia zimekimbilia kufuatia vurugu mpya mjini El Fasher.
Maelfu ya watu wanaaminika bado wamekwama katika mji wa El Fasher nchini Sudan, huku jamaa zao wakihangaika kutafuta taarifa zao. Swali kuu ni kujua ni watu wangapi bado wamebakia ndani ya mji huo. Hali hii ilianza mwezi uliopita baada ya mzingiro wa siku 500 katika mji mkuu wa Darfur Kaskazini.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia simulizi za waahirika wa Kimbunga Melissaikiwa ni wiki ya pili sasa baada ya kupiga magharibi mwa Jamaica, na kuacha zahma kubwa kwa wakaazi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema dunia haiwezi kuigeuzia kisogo Afrika akisisitiza kuwa bara hilo ni nyumbani kwa karibu robo ya watu wote duniani, na lina nafasi kubwa ya maendeleo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake (UN Women) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kukomesha ukatili na mateso yanayowakumba wanawake na wasichana nchini Sudan, likisema kuwa vita vinavyoendelea vimegeuka kuwa “vita dhidi ya wanawake.”
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya haki za binadamu nchini Sudan, Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) nchini Tanzania, na kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria.
Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetoa tamko juu ya wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti mpya kutoka El-Fasher, jimboni Darfur Kaskazini, nchini Sudan, zikieleza kuwepo kwa mauaji ya halaiki, ubakaji, na uhalifu mwingine unaodaiwa kufanywa wakati wa mashambulizi ya Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF). Taarifa zaidi na Sheilah Jepngetich.
Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetoa tamko juu ya wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti mpya kutoka El-Fasher, jimboni Darfur Kaskazini, nchini Sudan, zikieleza kuwepo kwa mauaji ya halaiki, ubakaji, na uhalifu mwingine unaodaiwa kufanywa wakati wa mashambulizi ya Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF).
Tangu kuanguka kwa jiji la El-Fasher mikononi mwa Rapid Support Forces (RSF) ambavyo ni vikosi vya waasi vya Sudan, maelfu ya raia wamekimbia jiji hilo. Wote wameripoti ukiukwaji wa haki za binadamu unaoendelea katika eneo hilo, kwa mujibu wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa (OHCHR), ambayo imetahadharisha kuwa kuna taarifa mpya zinazoendelea kujitokeza kuhusu ukatili uliofanywa wakati na baada ya kuanguka kwa jiji hilo la Darfur Kaskazini.