Viongozi wa jamii Sudan Kusini na UNMISS walaani vurugu dhidi ya raia na walinda amani
Viongozi wa kijamii nchini Sudan Kusini wameomba radhi kwa vitendo vya ghasia vilivyofanywa na vijana waliokuwa wamelewa katika kambi ya Umoja wa Mataifa ya kulinda raia mjini Bentiu ambapo raia wawili walifariki dunia na wafanyakazi wanane wa Umoja wa Mataifa kujeruhiwa wakiwemo maafisa wa polisi watano.