Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sola

02 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Sudan Kusini na mradi wa maji nchini Rwanda. Makala tunasalia huko huko Sudan Kusini na Mashinani tunakupeleka nchini Zimbabwe, kulikoni?  

Sauti
11'38"

16 DESEMBA 2022

Jaridani leo Ijumaa ya tarehe 16  ya mwezi Desemba mwaka 2022 tunakuletea habari kuhusu uhamiaji na kazi za walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.  

Sauti
11'31"
Wanaume wawili wakipakia paneli za jua kwenye boti ndogo katika Ziwa Turkana nchini Kenya.
Climate Visuals Countdown/Maurizio Di Pietro

Matumizi ya umeme wa Sola yawezesha huduma za mahakama kupatikana muda wote nchini Kenya

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na madawa ya kulevya na uhalifu UNDOC kanda ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na sekta ya mahakama nchini kenya wamepanga kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa uwekaji umeme wa sola katika mahakama na magereza nchini humo baada ya awamu ya kwanza kuonesha mafanikio.

26 AGOSTI 2022

Katika Jarida la habari za UN hii leo Flora Nducha anakuletea -Mradi wa maji safi na salama jimboni Cibitoke nchini Burundi kwa msaada wa UNICEF umeleta afuweni kwa wakazi na hasa watoto -Mkimbizi kutoka DRC anayeishi Kakuma Kenya ameleta nuru ya nishati ya sola kwa wakimbizi wenzie huku akijiingizia kipato -Makala leo inatupeleka Tanzania kumulika jitihada za vijana katika kupambana na ukimwi na afya ya uzazi kwa kuelimisha vijana Balehe -Na mashinani afisa wa shirika la afya duniani WHO nchini Senegal anaeleza changamoto za upatikanaji wa taarifa za afya Afrika
Sauti
11'51"
Kilimo nchini Bangladesh
© WFP/Sayed Asif Mahmud

Mradi wa umwagiliaji wa sola wawanufaisha wakulima na kuokoa mazingira Bangladesh:FAO 

Nchini Bangladesh uhaba wa maji unatishia uzalishaji wa kilimo na maisha ya wakulima hasa kutokana na kutokuwa na mifumo bora ya uwagiliaji ambayo inasababisha upotevu wa maji. Lakini sasa changamoto hizo zinageuka historia baada ya shirika la chakula na kilimo FAO kuanzisha mradi wa mifumo bora ya umwagiliaji inayotumia nishati ya jua au sola kunusuru wakulima na mazingira.

Sauti
2'37"