07 AGOSTI 2023
Hii leo jaridani tunaangazia mizozo Sudan na ukulima wa mboga mboga nchini Benin. Makala tunakupeleka nchini Mauritius na mashinani nchini Kenya, kulikoni?
Hii leo jaridani tunaangazia mizozo Sudan na ukulima wa mboga mboga nchini Benin. Makala tunakupeleka nchini Mauritius na mashinani nchini Kenya, kulikoni?
Nchini Benin, mradi unaofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji, UNCDF umewezesha vijana waliokuwa wanazurura wakati wa msimu wa mwambo nchini humo kuweza kuendelea na shughuli za kilimo kutokana na mradi huo kuwapatia pampu za kusukuma maji ya umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Sudan Kusini na mradi wa maji nchini Rwanda. Makala tunasalia huko huko Sudan Kusini na Mashinani tunakupeleka nchini Zimbabwe, kulikoni?
Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, IOM linasaidia kuhamishia nchini Rwanda, wasichana kutoka Afghanistan ili waweze kuendelea na elimu, kufuatia uamuzi wa serikali iliyojiweka madarakani nchini mwao kupiga marufuku wanawake na wasichana kuendelea na elimu ya sekondari na ya juu nchini Afghanistan.
Jaridani leo Ijumaa ya tarehe 16 ya mwezi Desemba mwaka 2022 tunakuletea habari kuhusu uhamiaji na kazi za walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na madawa ya kulevya na uhalifu UNDOC kanda ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na sekta ya mahakama nchini kenya wamepanga kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa uwekaji umeme wa sola katika mahakama na magereza nchini humo baada ya awamu ya kwanza kuonesha mafanikio.
Katika ziara yake ya siku mbili nchini India, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alitembelea eneo la mradi wa mfano katika jimbo la Gujarat, lililoteuliwa kuwa kijiji cha kwanza cha nishati ya jua nchini humo.
Nchini Bangladesh uhaba wa maji unatishia uzalishaji wa kilimo na maisha ya wakulima hasa kutokana na kutokuwa na mifumo bora ya uwagiliaji ambayo inasababisha upotevu wa maji. Lakini sasa changamoto hizo zinageuka historia baada ya shirika la chakula na kilimo FAO kuanzisha mradi wa mifumo bora ya umwagiliaji inayotumia nishati ya jua au sola kunusuru wakulima na mazingira.
Nchini Yemen katika jimbo la kusini-magharibi, la Ibb, mbinu mpya za umwagiliaji kwa kutumia mradi wa kusukuma maji kwa nguvu za sola umeleta nuru mpya na matumaini kwa wakazi wa eneo hilo.