Shamra shamra za maadhimisho ya siku ya wanawake zamulikwa Afrika Mashariki
Katika makala hii tunamulika maadhimisho ya siku ya wanawake tujiunge na Anthony Joseph wa radio washirika Wapo Radion FM ya Tanzania na kisha John Kibego wa radio washirika Spice FM huko Uganda.
Siku ya wanawake duniani yamulikwa Maziwa Makuu Afrika
Tarehe Nane Machi kila mwaka ni siku ya wanawake duniani! Ujumbe wa mwaka huu ni Usawa kwa wanawake Maendeleo kwa Wote! Ujumbe huo umepigiwa chepuo kila kona ya dunia kwa kutambua kuwa iwapo wanawake watapatiwa fursa zaidi iwe katika sekta za kijamii, kiuchumi au kisiasa, manufaa yanayopatikana ni kwa jamii nzima. Hii ni kwa kuzingatia nafasi adhimu kwenye kaya zao na jamii kwa ujumla.