Ujasiriamali ni miongoni mwa mikakati bunifu ya kuwawezesha wanawake kuinuka kiuchumi wakati huu ambapo malengo ya maendeleo endelevu SDGs yanapigia chepuo uwezeshaji wa wanawake katika kila ngazi.
Wanawake wameshamiri juma hili. Mataifa mengi yameadhimisha siku ya wanawake duniani mnamo Machi nane, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka, lengo likiwa kupigia chepuo haki na ustawi wa kundi hilo katika nyanja mbalimbali.
Ukosefu wa teknolojia wezeshi unapunguza mapato kusudiwa kwa wanawake mkoani Kagera nchini Tanzania, hii ni kwa mujibu wa wajasiriamali mkoani humo ambao wanasema wakiwezeshwa kiteknolojia watazalisha maradufu.