Chuja:

Siku ya usaidizi wa kibinadamu

© UNOCHA/Matteo Minasi

Yahitaji 'kijiji' kusaidia walio kwenye majanga - Guterres

Hii leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya utoaji wa misaada ya kibinadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amepazia sauti watoa huduma za kibinadamu ambao hufanya kazi kutwa kucha a hasa kwa wale wanaopitia majanga wanaojikuta wao wenyewe wakibeba jukumu la kutoa msaada ili dunia iwe pahala bor
 
Katika ujumbe wake aliotoa kwa njia ya video hii leo, Katibu Mkuu ametumia methali isemayo yahitaji Kijiji kukuza mtoto, akiongeza kuwa yahitaji pia Kijiji kusaidia watu wanaokumbwa na majanga ya kibinadamu. 

Sauti
2'3"

19 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunamulika siku ya kimataifa ya usaidizi wa binadamu duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anatoa shukrani kwa wale wote wanaojitolea kuchukua hatua kusaidia wengine hata wenyewe wakiwa bado na shida, huku akikumbuka wale waliopoteza maisha wakisaidia wengine. Tunakwenda pia Mexico huko ambako taka za mwani zinatengeneza matofali. Makala tunabisha hodi Kigoma, Leah Mushi anakuletea simulizi ya wanawake wanufaika wa miradi inayotekelezwa na UNDP chini ya KJP. Mashinani ni wito kutoka kwa Mkuu wa WHO ili kusaidia wakazi wa jimbo la Tigray nchini Ethiopia.

Sauti
11'48"