Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Kwenye mji mkuu wa Dd'jamena Chad, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 17 akitabasamu baada ya kupimwa na kubainika kuwa hana VVU.
© UNICEF/Frank Dejong

Usawa ndio jawabu mujarabu la kutokomeza VVU na Ukimwi- WHO

Ikiwa leo ni siku ya Ukimwi duniani maudhui yakiwa kumaliza ukosefu wa usawa ili kila mtu aweze kupata huduma za kujikinga au kupunguza makali dhidi ya Virusi Vya Ukimwi, VVU na Ukimwi, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, kanda ya Afrika limesema maudhui hayo yamekuja wakati muafaka kwa kuwa ukosefu wa usawa ndio chanzo cha kuibuka na kusambaa kwa magonjwa ya milipuko na yaliyojikita mizizi barani Afrika.