Skip to main content

Chuja:

SIKU YA UKIMWI DUNIANI

1 DESEMBA 2022

Leo ni Siku ya Ukimwi duniani na jarida linakuletea mada kwa kina tukijikita kabisa nchini Nigeria, moja ya nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara ambako ripoti inasema hali si shwari ya maambukizi.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi na mashinani  

Sauti
13'4"
Mwanamke aliyezaliwa na VVU akipokea dawa kwenye kliniki nchini Burkina Faso
© UNICEF/Frank Dejongh

Ili kuumaliza UKIMWI lazima tuweke usawa duniani kote – Katibu Mkuu UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa Siku ya UKIMWI Duniani, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe Mosi Desemba, amesema ili kuumaliza ugonjwa huo lazima kwanza kukomesha ukosefu wa usawa ambao unakwaza hatua za kusonga mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu unaohatarisha maisha ya watu ulimwenguni kote.

Kwenye mji mkuu wa Dd'jamena Chad, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 17 akitabasamu baada ya kupimwa na kubainika kuwa hana VVU.
© UNICEF/Frank Dejong

Usawa ndio jawabu mujarabu la kutokomeza VVU na Ukimwi- WHO

Ikiwa leo ni siku ya Ukimwi duniani maudhui yakiwa kumaliza ukosefu wa usawa ili kila mtu aweze kupata huduma za kujikinga au kupunguza makali dhidi ya Virusi Vya Ukimwi, VVU na Ukimwi, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, kanda ya Afrika limesema maudhui hayo yamekuja wakati muafaka kwa kuwa ukosefu wa usawa ndio chanzo cha kuibuka na kusambaa kwa magonjwa ya milipuko na yaliyojikita mizizi barani Afrika.