22 MACHI 2022
Jaridani leo tunaangazia mkutano wa maji hapa makao makuu na kusalia kwenye siku ya maji tukimulika upatikanaji wa maji nchini DRC. Makala na mashinani tutasalia huko huko DRC, kulikoni?
Jaridani leo tunaangazia mkutano wa maji hapa makao makuu na kusalia kwenye siku ya maji tukimulika upatikanaji wa maji nchini DRC. Makala na mashinani tutasalia huko huko DRC, kulikoni?
Mkutano wa maji wa Umoja wa Mataifa unaanza leo ukibeba maudhui “kushikamana kwa ajili yam aji kwa wote” Ikiwa pia ni siku ya maji duniani na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kuchukuliwa hatua madhubuti sasa ili kuhakikisa rasilimali hiyo adhimu inalindwa, kudhibitiwa ipasavyo na kupatikana kwa kila mtu.
Mkutano wa maji wa Umoja wa Mataifa unaanza leo ukibeba maudhui “kushikamana kwa ajili ya maji kwa wote” ikiwa pia ni siku ya maji duniani na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kuchukuliwa hatua madhubuti sasa ili kuhakikisa rasilimali hiyo adhimu inalindwa, kudhibitiwa ipasavyo na kupatikana kwa kila mtu.
Yaliyomo Jaridani la Jumanne Machi 22, 2022- Ujenzi wa mabwawa waboresha maisha ya wakulima wa mbogamboga nchini Rwanda.
-Sindano mpya ya Cabotegravir kutusaidia kukinga wengi dhidi ya VVU:UNITAID.
-UNHCR inahitaji dola bilioni 1.2 kwa ajili ya ktoa msaada kwa wakimbizi milioni 2.3.
Makala imeangazia mjadala wa wakulima wadogo wadogo kutoka Afrika.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mastaifa Antonio Guterres ametoa rai kwa dunia kuchukua hatua sasa ili kuilinda na kuienzi rasilimali maji kwa ajili ya kizazi hiki na mustakbali wa kizazi kicjacho wakati huu rasilimali hiyo ikizidi kuwa adimu.
Ikiwa leo ni siku ya maji duniani (22 Machi) nchini Rwanda mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kilimo na Chakula FAO wa ujenzi wa mabwawa umebadilisha maisha ya wakulima wa mboga mboga kwa kuwaongezea kipato na pia kuwapatia maji safi na salama.
Ingawa virusi vya corona au COVID-19 katika wiki za hivi karibuni vimekuwa vikichukua nafasi kubwa katika habari, hatupaswi kusahau moja ya matishio makubwa kwa ubinadamu: madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa dunia, Umoja wa Mataifa umetoa wito katika ripoti mpya kuhusu maji.
Maji ni muhimu sana kwa uhai wa mtu sanjari na usafi vinasaidia kulinda afya ya jamii na mazingira. Amesema hayo hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya maji duniani ambayo kila mwaka huadhimishwa Machi 22.
Ikiwa leo ni siku ya maji duniani, maudhui yakiwa hakuna kumwacha mtu nyuma katika kupata huduma hiyo ifikapo mwaka 2030 kwa kuzingatia lengo namba 6 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, Tanzania imetaja hatua iliyochukua ili kufanikisha lengo hilo.
Suala la rasilimali ya maji ni la uhai au mauti na si suala la kulifanyia lele mama. Dunia lazima ishikamane kudhibiti matumizi ya rasilimali hii ili kupunguza uhaba wake amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa antonio Guterres leo, ikiwa ni siku ya maji duniani.