Siku ya haki za binadamu

Siku ya UN, wakimbizi Uganda wapaza sauti

Ikiwa leo ni siku ya Umoja wa Mataifa, makundi mbalimbali yamezungumzia kile ambacho chombo hicho kinawasaidia katika zama za sasa zilizogubikwa na changamoto lukuki. Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193 unahakikisha kuwa rasilimali kidogo iliyopo inatumika kuleta maisha bora hata kwa watoto na vijana wakimbizi ambao kwao maisha ni machungu na hivyo wamekimbilia ugenini. Mfano ni nchini Uganda ambako katika siku hii ya Umoja wa Mataifa, John Kibego amevinjari na kuzungumza nao.

Sauti
3'23"

Chukua hatua, simamia haki za binadamu:Zeid

Leo ni siku ya kimataifa ya haki za binadamu duniani ambayo kila mwaka huadhimishwa tarehe 10 ya mwezi Desemba. Mwaka huu ikiwa ni wa 69 tangu kupitishwa kwa azimio namba 2017  la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa hapo Desemba mwaka 1948, Kamisha mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Zeid Raa’d al Hussein ametoa ahadi ya kuhakikisha haki hizo zinapiganiwa na kuheshimiwa