Weka haki za binadamu katika kitovu cha juhudi za kubadili mwelekeo wa leo wa uharibifu - Guterres
Ikiwa leo ni Siku ya Haki za Binadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia ujumbe wake mahususi kwa ajili ya siku hii amesema, "Nyakati za majaribu" za leo zinaeleza hitaji la kujitolea tena kwa haki za binadamu, ambazo ni muhimu katika kutatua matatizo ya kimataifa.