Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sierra Leone

Wahudumu wa afya Sierra Leone wakifundishwa matumizi ya vifaa vya kielektroniki katika usimamizi na ufuatiliaji wa magonjwa na afya.
WHO/Saffea Gborie

WHO Afrika ilivyoisaidia Sierra Leone kuwa kinara wa kugundua magonjwa ya mlipuko

Kati ya mwaka 2014 mpaka 2016 kulitokea mlipuko wa ugonjwa mbaya zaidi wa Ebola katika nchi ya Sierra Leone na nchi jirani, mlipuko uliogharimu maisha ya zaidi ya wanawake, wanaume na watoto 4000 katika nchi hiyo. Wizara ya Afya ya nchi hiyo inaeleza kuwa tukio hilo la mlipuko wa Ebola lilikuwa la kushtukiza kwani walikuwa wana mfumo wa kawaida wa ufuatiliaji kwa kutumia karatasi au ujumbe mfupi kwa njia ya simu hali iliyofanya kupata taarifa kwa wakati kuwa chini ya asilimia 40. 

Sauti
4'30"
© WHO/Michael Duff

Mifumo madhubuti ya kuwasiliana Sierra Leone imeimarisha uthibiti wa milipuko ya magonjwa

Takriban miaka 10 iliyopita nchi kadhaa za Afrika zilikumbana na mlipuko wa ugonjwa hatari wa ebola uliogharimu maisha ya mamilioni ya watu. Moja ya nchi hizo ni Sierra Leone ambayo wakati mlipuko wa Ebola ukiikumba nchi hiyo walikuwa hawana njia bora za kuwasiliana kama taifa na kujua ukubwa wa ugonjwa huo na namna ya kudhibiti. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika mbali na kuisaidia nchi hiyo kupamba na Ebola lakini iliwasaidia kuweka mifumo madhubuti ya kuwasiliana nchi nzima kujua iwapo kuna mlipuko wa ugonjwa wowote.

Sauti
4'30"

03 FEBRUARI 2023

Hii leo jaridani tunamulika elimu, watu wenye ulemavu, saratani ya shingo ya kizazi na ujumbe kuhusu harakati za kutokomeza ukeketaji wa wanawake na wasichana, FGM. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.

Sauti
12'8"
IFAD

Wakulima wenye ulemavu nao wanaweza kujipatia kipato

Inakadiriwa kuwa asilimia 20 ya watu maskini zaidi duniani wana aina fulani ya ulemavu. Watu wa vijijini wanaoishi na ulemavu wanakabiliwa na changamoto zaidi kuliko wenzao wa mijini ndio maana ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu ni lengo muhimu katika kutekeleza azma ya Mfuko wa umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD. 

IFAD tayari ina uzoefu katika kufanya kazi na watu wenye ulemavu. Katika miaka ya hivi karibuni, IFAD imekuwa ikiongeza juhudi zake za kuwajumuisha watu wote wenye ulemavu. 

Sauti
3'53"