Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

shirikalawakimbizi

Dondakoo wasalia “mwiba” Yemen- WHO

Ugonjwa wa dondakoo unazidi kuwa tishio nchini Yemen baada ya kubainika kuwa hadi sasa hakuna chanjo dhidi ya ugonjwa huo kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka mitano na kuendelea pamoja na vijana.

Shirika la afya duniani WHO linasema ingawa dozi 100,000 za kutibu dondakoo ziliwasili Jumatatu, dawa hizo ni kwa watoto walio na chini ya umri wa miaka mitano.

WHO imetaka hatua zaidi za kufungua mipaka ili misaada ya kibinadamu pamoja na dawa ziwafikie walengwa haraka ikwezekanavyo.