Chuja:

shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii duniani

Idadi ya watalii duniani ilipanda 2017 na huenda ikaongezeka zaidi :UNWTO

Idadi ya watalii wa kimataifa, wanaowasili katika nchi nyingine, na watu wanaoingia nchi moja kwa siku kwa njia  halali iliongezeka mwaka wa 2017 kwa kiwango cha asili mia 7 na na hivyo  kufikia watalii Zaidi ya millioni elfu moja na mia tatu.

Hii ni kwa mujibu wa vigezo vipya vya shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii duniani UNWTO. Shirika hilo linabashiri kuwa ongezeko hilo litazidi kuvuma mwaka 2018 kwa kiwango cha asili mia  kati ya nne na tano.