Skip to main content

Sheria na kuzuia uhalifu

UN Kenya/Newton Kanhema

UN yapongeza Kenya kwa kutumia sheria ya kimataifa kushtaki watuhumiwa wa uhalifu baada ya uchaguzi mkuu 2017

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017. Leah Mushi anataarifa zaidi.

Sauti
1'59"
Al Hassan akiwa mbele ya mahakama ya ya kimataifa ya uhalifu, ICC mnamo Aprili 4, 2018
ICC-CPI

Al Hassan anayo kesi ya kujibu-ICC

Baraza la rufaa la Mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC limeitupilia mbali rufaa iliyokuwa imeletwa mbele yao na  Al Hassan kupinga uamuzi wa awali wa kumpata na kesi ya kujibu kuhusu makosa anayodaiwa kuyatenda katika eneo la Timbuktu nchini Mali kati ya mwaka 2012 na 2013.