Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

shambulio

Rosemary DiCarlo akitoa taarifa kwenye Baraza la Usalama kuhusu shambulio la Israel Doha Qatar
UN Photo/Loey Felipe

Shambulio la Israel Doha Qatar laleta mshtuko, UN yataka diplomasia iheshimiwe

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo lilipewa taarifa na afisa mkuu wa masuala ya siasa wa Umoja wa Mataifa kuhusu shambulio la anga la Israel mjini Doha Qatar na kusema ni ongezeko la kutisha la mvutano lililolaaniwa kama uvunjaji wa mamlaka ya nchi unaotishia mazungumzo yanayoendelea ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka huko Gaza.

© UNICEF/Aleksey Filippov

Umoja wa Mataifa imelaani vikali shambulio lililoua na kujeruhi wafanyakazi wa ukoaji Kherson Ukraine

Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Ukraine Matthew Hollingworth amelaani vikali shambulio lililofanywa na Urusi kwenye eneo la Kherson lililoathirika vibaya na mafuriko ya bwawa la Kakhovka, na kukatili maisha ya mfanyakazi wa ukoaji na kujeruhi wengine. 

Katika tarifa yake iliyotolewa leo mjini Kyiv  Ukraine mratibu huyo Hollingworth amesema “Inasikitisha sana kwamba waokoaji wameuawa na kujeruhiwa jana huko Kherson walipokuwa wakisaidia jamii zilizoathiriwa na uharibifu mkubwa wa bwawa la Kakhovka.”

Sauti
1'39"
Wakimbizi kutoka Burundi wakichota maji katika kambi ya Lusenda, Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, DRC.
UNHCR/Colin Delfosse

Mlinda Amani wa Umoja wa Mataifa auwawa nchini DRC

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio lililotokea hapo jana tarehe 30 Septemba 2022 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC katika kambi ya COB iliyopo chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na kusababisha kifo cha mlinda amani mmoja raia wa Pakistan.

Mtoto akitembea katika kambi ya muda ya Kabul baada ya familia yake kuyakimbia makazi yao kutokana na mzozo nchini Afghanistan
© UNICEF Afghanistan

Shambulio la kigaidi Kabul ni msumari wa moto juu ya kidonda kwa Waafghanistan:UN

Ofisi ya Kamisnina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa imesema shambulio la kigaidi lililofanywa na kundi la ISIL-Khorasan kwenye uwanja wa Ndege wa Kabul nchini Afghanistan jana ni ililikuwa hatua na uamuazi mbaya wa kundi hilo, nani bayana lilikuwa limepangwa kuua na kulemaza watu wengi iwezekanavyo wakiwemo raia, watoto, wanawake, kina baba, kina mama, pamoja na Taliban na vikosi vya kigeni vinavyolinda uwanja wa ndege.