UN yatoa wito wa ushirikiano wa kimataifa kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kufikia SDGs
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiongea leo katika mkutano muhimu wa ushirikiano wa kimataifa, amesema ikiwa serikali zitaafikiana kwa pamoja malengo ya kumaliza makaa ya mawe, kuongeza ahadi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuwekeza katika malengo ya dunia, kuna fursa ya kuishinda "changamoto kubwa ya maisha yetu".