Juhudi za kidiplomasia zinaendelea katika Baraza la Usalama na katika miji mikuu ya nchi mbali mbali kujaribu kutafuta suluhisho la kusitisha mapigano kati ya Israel na wapiganaji wa Hezbollah huko Lebanon.
Afisi ya kulinda amani ya UM huko Burundi ONUB imeeleza kushangazwa na ripoti kua kulikuwepo na jaribio la kuipindua serekali ya Bujumbura, siku chache zilizopita na kwamba kuna wanasiasa mashuhuri walotiwa vizuizini.