Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

SDG14

Kadir van Lohuizen/NOOR/UNEP

Jamii zilizo jirani na bahari ni wadau wakuu katika kulinda bahari- Soares

Baada ya siku tano za mijadala na maonesho mbalimbali, mkutano wa pili kuhusu baharí umefikia tamati huko Lisbon nchini Ureno ambako Miguel de Serpa Soares ambaye ni Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya kisheria amesema mwelekeo wa kulinda na kuhifadhi baharí unatia matumaini kwa kuzingatia yaliyokubaliwa, changamoto zilizoko sambamba na fursa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
1'54"
Ocean Image Bank/Vincent Knee

Tuilinde bahari ili itulinde- Guterres

Mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon Ureno ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni lazima kubadili mwelekeo na mwenendo wa shughuli za binadamu kwa bahari la sivyo uchafuzi wa bahari utavuruga  harakati zote za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Ndivyo alivyokuwa anatamatisha hotuba yake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo huko Lisbon kwa lugha ya kiswahili kwenye mkutano huo wa baharí ulioandaliwa kwa pamoja na Kenya na Ureno.

Sauti
2'3"
Ufunguzi wa mkutano kuhusu bahari huko Lisbon, Ureno 27 Juni 2022
UN /Eskinder Debebe

Bahari inatupeleka popote, tuitunze- Guterres

Mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon Ureno ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni lazima kubadili mwelekeo na mwenendo wa shughuli za binadamu kwa bahari la sivyo uchafuzi wa bahari utavuruga harakati zote za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs

Sauti
2'3"
Coral Reef Image Bank/Jayne Jenk

Harakati za kuhifadhi matumbawe zazaa matunda

Matumbawe, hupatikana kwenye zaidi ya nchi 100 duniani kote ikiwemo nchi za visiwa vidogo, SIDS na mataifa mengine yanayoaendelea. Licha ya umuhimu wake katika kusaidia uhai ndani ya bahari, matumbawe yako hatarini kutoweka kutokana na shughuli za binadamu zinazochochea mabadiliko ya tabianchi. Umoja wa Mataifa unasema kuwa theluthi mbili za matumbawe duniani ziko hatarini na ndio maana lengo namba 14 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi na matumizi endelevu ya bahari na rasilimali zake kwa ajili ya maendeleo endelevu. Je nini kinafanyika?

Sauti
4'23"

Plastiki za kutumia na kutupa si mtaji!

Baada ya kushiriki na kufanikisha mafanikio ya kampeni ya kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki nchini Kenya, mwanaharakati na mpiga picha nchini humo James Waikibia amesema hivi sasa ameelekeza nguvu zake kwenye kutokomeza matumizi ya vifaa vya plastiki vinavyotumika mara moja na kutupwa.

Vifaa hivyo ni pamoja na vijiko, umma, sahani na visu ambayo matumizi yake yameshamiri sana hivi sasa kila kona duniani.

Bwana Waikibia katika mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amesema amejikita kutokomeza matumizi ya vifaa hivyo nchini Kenya kwa kuwa..

Audio Duration
1'38"