UNHCR imeturejeshea matumaini ya maisha: mkimbizi Muhammad toka Eritrea
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limerejesha matumaini ya maisha kwa wakimbizi kutoka Eritrea Muhammed na mkewe Mariam ambao baada ya kupitia milima na mabonde kwa zaidi ya miaka 10 ukimbizini sasa wako tayari kwenda kuanza upya maisha nchini nchini Uholanzi kupitia mpango wa shirika hilo wa kuwapa makazi ya kudumu wakimbizi katika nchi ya tatu.