Maelfu wanaendelea kufungasha virago Ituri, DRC na kumiminika Uganda
Shirika la Umoja w aMataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), limeripoti kuwa wakimbizi takribani 4,000 wamekimbilia Uganda kufuatia kushamiri kwa mzozo wa kikabila Jimbo la Ituri na mashambulizi ya vikundi vilivyojihami Jimboni Kivu Kaskazini katika kipindi cha wiki moja tu.