Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Roboti

06 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Eugene Uwimana mmoja wa maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini Rwanda amemtembelea mhamasishaji wa lugha ya Kiswahili nchini humo Profesa Pacifique Malonga ambaye ameanzisha eneo maalumu la vitabu vya Kiswahili katika Maktaba Kuu ya mji wa Kigali. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za uhamiaji, usafirishaji haramu wa binadamu na Akili Bandia. Katika jifunze Kiswahili hii leo tunabisha hodi kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA kupata ujumbe maalum kuhusu umuhimu wa lugha.  

Sauti
12'10"
UN RWANDA

Roboti zawapunguzia kazi watoa huduma za afya nchini Kenya

Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP nchini Kenya linaendesha programu ya majaribio ya kutumia roboti ili kupima afya za wasafiri wanaoingia na kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, pamoja na Hospitali Kuu ya Taifa ya Kenyatta, lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kuwapunguzia mzigo watendaji wa sekta ya afya. Leah Mushi anataarifa zaidi. 
 
(Taarifa ya Leah Mushi) 

Sauti
2'13"
Uwezo bandia unafungua milango katika kuboresha huduma ya afya ulimwenguni.
Unsplash/Possessed Photography

Roboti uwanja wa Jomo Kenyatta zapima COVID-19 na kufukiza dawa 

Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP nchini Kenya linaendesha programu ya majaribio ya kutumia roboti katika kupima afya za wasafiri wanaoingia na kutoka katika uwanja wa ndege wa kimataifa Jomo Kenyatta jijini Nairobi pamoja na Hospitali Kuu ya Taifa ya Kenyatta lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kuwapunguzia mzigo watendaji wa sekta ya afya.

Sauti
2'13"
UN/ Jason Nyakundi

Vijana waunda roboti ya kusaidia watu wenye ulemavu

Hawana kisomo cha chuo kuu lakini ujuzi wao katika masuala ya teknolojia ya kuunda roboti inayoweza kusoma na kuelewa anachofikria mwanadamu na ni uvumbuzi ambao umewashangaza wengi. Moses Njoroge na David Gathu ni wavumbuzi walio na karakana yao ndogo eneo la Kikuyu kaunti ya Kiambu nje kidogo ya mji wa Nairobi nchini Kenya, ambapo kwa kipindi cha miaka 10 wamejikita katika kuunda roboti inayoweza kuwasaidia watu walio na ulemavu wa miguu na mikono kujihudumia. Mwandishi wetu nchini Kenya Jason Nyakundi amezungumza nao akianza na Moses.
 

Sauti
4'35"