Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

review-audio-programme

Njombe wafurahia usaidizi wa UN

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo, UNDP Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo kutoka Uingereza, Marekani na Sweden  na serikali ya Tanzania linajitahidid kutekeleza mpango wa kunusuru kaya masikini (PSSN) kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), ambao kwa sasa umefikia takriban kaya milioni 1.1 wenye umasikini uliokithiri nchini humo...

Sauti
3'31"
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Kina mama wajasiriamali waneemeka na mafuta Uganda

Upatikanaji wa bidhaa ya mafuta nchini Uganda umeleta faraja kwa mamilioni ya wananchi ambao sasa wanaona nuru ya kupungua kwa bei ya bidhaa hiyo katika siku za usoni. Na neema hiyo sio kwa waendesha magari tu bali pia kwa wafanya biashara ndogondogo au wajasiriamali wakiwemo wanawake. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amewatembelea baadhi ya wanawake walioanza kunufaika na uwepo wa shughuli za uchimbaji mafuta katika eneo la ziwa Albert nchini humo ili  kupata ufafanuzi zaidi unagana naye

Picha: UNPA

Wasichana Sierra Leone wapingana na wazazi kulinda haki zao

Hebu fikiria mtoto wa kike punde tu baada ya kuzaliwa anafungwa kamba mkononi, ya kwamba ni kishika uchumba kwa kuwa tayari amepata mume. Hiyo inaweza isikuingie akilini iwapo u mkazi wa nchia ambako haki za mtoto zinazingatiwa, hata hivyo nchini Sierra Leone, hilo ni jambo la kawaida na linapatiwa msisitizo kutokana na ukatili wa kijinsia na mila na desturi potofu. Hata hivyo hivi sasa nchini humo wapo watoto wa kike na wasichana ambao wamefunguka macho na wanapingana na hata wazazi wao. Je wanafanya nini?

Sauti
4'12"

Dansi ya kitamaduni yaenziwa Uganda

Wakati shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO), linapigia chepuo utunzaji na ukuzaji wa utamaduni,  mjini Hoima nchini Uganda, waimbaji wa kitamaduni waliandaa tamasha la muziki kandoni mwa tamasha za muziki wa kisasa.

Je, lilishindana? Basi ungana na John Kibego katika makala ifuatayo...

Ufugaji nyuki sasa ni mtaji dhidi ya umaskini huko Kyela, Tanzania

Kupitia lengo namba moja la kutokomeza umasikini lililomo kwenye ajenda ya  maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa  ya mwaka 2030, serikali zinahimizwa kutafuta mbinu mbadala kuwawezesha wananchi kupitia miradi mbalimbali ili kujikwamua na umasikini ifikikapo mwaka 2030.

Tanzania ni nchini mojawapo ambako serikali imechukua jukumu la kutoa elimu ya SDGs kwa kutafsiri malengo yao endelevu kwa lugha ya kiswahili ili kutoa mwongozo kwa wananchi na pili kuwapatia fursa za ujasiriamali kupitia miradi  mbalimbali kama  ufugaji, uvuvi, kilimo na kadhalika.