Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

RDC

Viongozi wa wanawake DRC wakiwakilisha  sekta zote za asasi za kiraia, wakiwa na Leila Zerrougui, Mkuu wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, MONUSCO
MONUSCO/John Bompengo

Inasikitisha baadhi ya raia wa DRC hawatashiriki uchaguzi huu muhimu-Bi Zerrougui

Leila Zerrougui, Mwakilishi Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, amesema kuwa anasikitika kwamba kuna raia ambao hawataweza kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaofanyika jumapili hii ya tarehe 30 mwezi huu wa Desemba nchini humo, kufuatia uamuzi wa Tume Huru ya Taifaya uchaguzi ya nchi hiyo, CENI, kuahirisha upigwaji kura katika maeneo ya Beni, Butembo na Yumbi kwa sababu ya mlipuko wa Ebola na ukosefu wa usalama.

 

MONUSCO yajenga uwezo polisi kuelekea uchaguzi mkuu DRC

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO unaendesha mafunzo ya kujengea uwezo wasimamizi wa uchaguzi pamoja na polisi nchini humo wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.

Mkuu wa kitengo cha polisi, MONUSCO Kamishna Mkuu Awalé Abdounasir, amesema mafunzo hayo yanayofanyika kwenye mji mkuu Kinshasa, yanalenga kuhakikisha polisi wanazingatia sheria na kanuni wakati wa kipindi cha uchaguzi.

Guterres kuzungumza na Rais Magufuli wa Tanzania

Kufuatia mauaji ya walinda amani 14 wa Tanzania huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC siku ya Alhamisi na wengine zaidi ya 44 kujeruhiwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres muda wowote sasa atazungumza kwa njia ya simu na Rais John Magufuli wa Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nchini Tanzania, Balozi Augustine Mahiga amesema hayo akihojiwa na Idhaa hii kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam.

(Sauti ya Balozi Augustine Mahiga)