Inasikitisha baadhi ya raia wa DRC hawatashiriki uchaguzi huu muhimu-Bi Zerrougui
Leila Zerrougui, Mwakilishi Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, amesema kuwa anasikitika kwamba kuna raia ambao hawataweza kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaofanyika jumapili hii ya tarehe 30 mwezi huu wa Desemba nchini humo, kufuatia uamuzi wa Tume Huru ya Taifaya uchaguzi ya nchi hiyo, CENI, kuahirisha upigwaji kura katika maeneo ya Beni, Butembo na Yumbi kwa sababu ya mlipuko wa Ebola na ukosefu wa usalama.