Urithi wa DRC ni wa watu wa DRC, tuhakikishe ni chanzo cha maendeleo na sio migogoro:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema utajiri na urithi wa rasilimali zilizosheheni nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ni wa watu wa Congo na si vinginevyo n ani jukumu la kanda nzima na jumuiya ya kimataifa kuhakikisha unakuwa chanzo cha maendeleo na mafanikio na sio vita.